AGIZO LA RAIS KUHUSU UKEKETAJI LATILIWA SHAKA
Serikali ya Kenya chini ya uongozi wa Rais Uhuru Kenyattaa iliahidi kuangamiza kabisa tabia ya ukeketaji wa wanawake hapa nchini ifikapo mwaka wa 2022.Mwanahabari wetu Philip Miyawa alitembelea vijiji vya Kuria katika county ya Migori ambapo tabia hii bado imekita mizizi miongoni mwa jamii na kutathmini juu ya uwezekano wa jamii hiyo kuwachana na mila hii potovu ifikapo mwaka ujao.